Nav bar

Alhamisi, 4 Aprili 2019

ZOEZI LA UOGESHAJI WA MIFUGO KANDA YA KATI

WIZARA ya mifugo na uvuvi, imeandaa mikakati ya kuboresha sekta ya mifugo hapa nchini, moja ya mkakati huo ni ule wa kudhibiti magonjwa ya mifugo ambapo imewahimiza wafugaji kuzingataia matumizi ya majosho yenye dawa za kuogesha ng’ombe ili kutokomeza magonjwa yatokanayo na kupe.

Hayo yalielezwa hivi karibuni na Naibu Waziri wa mifugo na uvuvi Mheshimiwa Abdalah Ulega wakati wa zoezi la uhamasishaji wa uogeshaji wa ng’ombe kanda ya kati mkoani Singida, katika kijiji cha Mgori kilichopo halmashauri ya wilaya ya Singida vijijini.

Katika uhamasishaji huo waziri Ulega aliwataka wafugaji kufanya zoezi la uogeshaji wa mifugo uliyoanzishwa uwe wenye tija na endelevu, kwa vile hivi sasa hakuna sababu za kushindwa kuogesha mifugo  yao katika majosho yenye dawa ya kudhibiti  kupe yaliyotolewa na serikali bure.

Alisema hivi sasa serikali katika zoezi hili, imetoa dawa bure kwa halmashauri zote nchini, na kukarabati majosho yote yaliyokuwa hayafanyi kazi, ili wafugaji waweze kuogesha mifugo yao, kukinga ugonjwa hatari unaoenezewa na kupe, ambao unaoongozwa katika vifo vya ng’ombe hapa nchini.

Hapo, mwanzo shughuli hizo zilikuwa zikifanywa kwa kutofuata taratibu nzuri za makusanyo yalikuwa yakitoka kwa wafugaji walipokuwa wakipata huduma za kuogesha mifugo yao, hazikuwa na taarifa ya mapato na matumizi na hivyo kushindwa kuwa na utaratibu endelevu wa shughuli hiyo, majosho mengi yalisimama kufanya kazi na mifugo haikugoeshwa.

Katika kampeni hii ya uhamasishaji wa uogeshaji wa mifugo, tozo imepunguzwa ambapo hivi sasa kila ng’ombe anaogeshwa katika majoshi ni shilingi 50 tu, huku nyuma uogeshaji ulikuwa unatozwa wastani wa shilling mia 200 kwa kila ng’ombe na kwa mbuzi ilikuwa shililngi 10.

“nyie wafugaji msikalie rasilimali hii ya mifugo mliokuwa mnayo, kwani ni uchumi mkubwa sana mliyokuwa nayo kwenu na pia kwa Taifa ili kuongeza mapato, yanayotokana na mifugo yenu” alisema mheshimiwa Ulega.

Aidha alifafanua kuwa ufugaji kwa kufuata taratibu za ufugaji wa kisasa na kibiahsra kwa kuvuna mifugo inapozidi katika eneo uliyokuwa nayo, itakusaidia kupata kipato katika kuboresha maisha yako na ya familia.  Uhamasishaji huu unafuatia uzinduzi wa kampeni ya uogeshaji wa mifugo, iliyofanywa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mh. Luhaga Mpina  katika kijiji cha Buzirayombo Halmashauri ya Chato Mkoa wa Geita.

Naibu Waziri Wa Mifugo Na Uvuvi Mh. Abdallah Ulega, katikati mwenye shati la rangi ya bluu  akiandaa dawa ya josho ili kuogesha mifugo

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni