Nav bar

Alhamisi, 4 Aprili 2019

MWEKEZAJI MKOANI MARA KUJENGA KIWANDA CHA NYAMA.




Mwekezaji katika sekta ya mifugo mkoani Mara, Mh. Vedastus Matayo, ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Musoma mjini, baada ya kutembelewa na Dawati la sekta binafsi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi ameamua kuanzisha kiwanda cha nyama mkoani hapo ili kuboresha soko la mifugo katika mkoa huo  na ajira watanzania.

Hayo yalibainishwa hivi karibuni na Mbunge huyo wakati alipotembelewa na Dawati la sekta binafsi  katika maeneo ya shughuli zake za ufugaji Wilayani Sengereti na Bunda, kwa lengo la kuibua na kushawishi kuwekeza kibiashara kwa Mbunge  huyo.

Mbunge huyo aliwambia wataalam hao wa Dawati kuwa ana mifugo aina, Ng’ombe zaidi ya 2000 aina ya Borani ambao ndiyo wengi na aina nyingine ya semental ambao ni wachache, mbuzi zaidi ya 2500 na kondoo zaidi ya 1000, mifugo yote hii iko wilaya za Bunda na Sengereti.

Aidha aliwaeleza aina ya ufugaji anaofuga wa kugoresha mifugo hiyo ya asili kwa njia ya uhimilishaji kwa kuchukua mbegu bora za mifugo toka NAIC Arusha na kuja kuchanganya na ng’ombe wetu majie wa asili ili kupata ng’ombe chotara mwenye uwezo wa kutoa nyama nyingi na maziwa mengi kuliko wale wa kienyeji.

Aliwaeleza wanadawati hilo la sekta  binafsi kuwa kwa kufanya hivyo ameweza zalisha mifugo mingi ambayo soko lake likawa ni changamoto, hivyo kuhitaji kuwa na kiwanda cha kuchakata nyama mkoa wa Mara.

Akizungumzia soko la mifugo hiyo baada ya kuizalisha kwa wingi na kuinenepeshamifugo hiyo alisema kuwa anauza kwa wenyeji wenye mabucha mkoani Mara na wakati mwengine huwauza nchi, nchini Kenya ng’ombe wa nyama.

Aidha kwa upande wa ng’ombe wa maziwa ambapo chotara hutoa maziwa mengi kiasi kuliko wale wa asili hufanya matumizi ya familia yake na wafanyakazi katika shughli zake za ufugaji na kilimo.

Kutokana na rasilimali hiyo kubwa aliyokuwanayo bwana Matayo ya mifugo na soko la mifugo hiyo ni changamoto kutegemea mkoa wa Mara tu na nchi jirani, dawati la sekta binafsi walimshauri kuanzisha kiwanda cha kuchakata nyama ili rasilimali ya mifugo mingi aliyo nayo ipate soko  katika kiwanda hicho.

Vilevile wataalam wa dawati walisema akianzisha kiwanda atazalisha bidhaa zitokanazo na nyama na kuziuza kwa bei yenye manufaa kwa vile atakuwa ameongeza thamani badala ya kuuza malighafi ya ng’ombe hai au mifugo hai, Mh. Matayo alikubaliana nao na kuahidiwa atapatiwa mkopo toka Banki ya maendeleo ya kilimo (TADB) na watashirikiana naye kuandaa andiko la mkopo huo wenye riba nafuu.



Mh. Mbunge wa Musoma mjini Mh. Vedastus Mathayo akiwa ofisini kwake akiongea na wataalamu wa dawati la sekta binafsi ambao hawaonekani pichani.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni