Nav bar

Jumatatu, 29 Oktoba 2018

SERIKALI YATEKETEZA NYAVU ZA WAVUVI HARAMU NYUMBA YA MUNGU


Serikali imepiga marufuku uvuvi haramu na kuteketeza nyavu aina ya makokoro 35 , makila 6 na nyavu za zenia 25 zilizokuwa zikitumiwa na wavuvi haramu katika bwawa la Nyumba ya Mungu lililopo Mkoani Kilimanjaro

Naibu Waziri wa mifugo na Uvuvi Abdalah Ulega akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kagongo kata Lang’ata leo amesema serikali haitamwonea huruma mtu yeyote atakayekamatwa akijihusisha na uvuvi haramu kwani serikali imekua ikipoteza kiasi kikubwa cha mapato kutokana na uvuvi huo.

“Hatuna utani na mtu asiye na huruma na rasilimali za nchi hii, Tanzania ndio nchi yenye sehemu kubwa yenye maji kuliko sehemu nyingine lakini bado tunaagiza samaki kutoka nchini china, tumeagiza sato., perege hadi kibua wa kichina, tusipotokomeza leo bwawa litakuwa historia kwa vizazi vijavyo” amesema Ulega

Kwa upande wake mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mghwira alisema uwepo wa bwawa hilo
umekuwa msaada mkubwa kwa wananchi katika eneo hilo na sasa ni wakati wa wananchi kuwa walinzi kwa kila mmoja ili kutokomeza uvuvi haramu.

“Hebu leo amueni kabisa kwamba biashara ya samaki ndio mfumo wa maisha yenu, Ninyi mkifanya
hivyo sisi hatutahitaji kufunga hili bwawa , wakati wote tutahitaji kuongeza kizazi cha samaki na kuleta wataalamu kupima kiwango cha samaki tulichonacho” alisema Mghwira

Kwa upande wake Dismas Gondwe mkazi wa kijiji cha kigongo kata ya Lang’ata amesema uvuvi haramu katika bwawa hilo unatokana na kukosekana kwa utaratibu maalumu unaowaelekeza wavuvi kuendesha shughuli zao katika bwawa hilo.

Gondwe ameiomba serikali kuwawezesha wavuvi wa bwawa la Nyumba ya Mungu zana harali ambazo serikali inazitambua.


Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega akizungumza na wavuvi wa kijiji cha Kagongo kata ya Langata mkoani Kilimanjaro juu ya serikali kutokumuonea huruma mtu yoyote ambaye anajiusisha na shughuli za uvuvi haramu 
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega (wa kwanza kulia) kwa kushirikiana na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro , Anna Mghwira na  Mkuu wa Wilaya ya Mwanga Aatron  Mbogho wakiteketeza zana haramu zilizokuwa zikitumika katika uvuvi haramu kwenye Bwawa la Nyumba  ya Mungu.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni