Nav bar

Alhamisi, 19 Aprili 2018

MNADA WA UPILI WA PUGU KUWA MNADA WA KIMATAIFA-LUHAGA MPINA

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe Luhaga Joelson Mpina amesema kuwa mnada wa pugu utakarabatiwa na  kuwa mnada wa kimataifa utakaokuwa unahudumia wafanyabiashara kutoka nchi yoyote Africa na duniani kwa ujumla.

Tanzania Mungu ametujalia kuwa na tunu ya Rasilimali ng'ombe,Nchi zilizoendelea wanajivunia  vitu vyao,Mfano viwanda,ifike wakati na Sisi tujivunie Rasilimali ng'ombe tuyoliyopewa Mungu Bure.

"Haiwezekani Sisi Tanzania tuwe wa pili africa kuwa na Mifugo mingi,tukitanguliwa na nchi ya Ethiopia halafu tukose kuwa  na mnada wa kimataifa"

Mpina ameyasema hayo Leo alipofanya ziara ya kukagua eneo la mnada huo lililovamiwa na wananchi na kujionea hali halisi ya uvamizi wa  eneneo hilo.

Pia baada ya kuzungu na kukagua eneo la mnada huo na kushuhudia uvamizi mkubwa uliofanyika katika eneo hilo,Mhe.Mipina ameunda timu maalumu itakayopita nyumba baada ya nyumba kuchunguza na kuhoji uhalali wao wa kuwepo katika eneo la Serikali na kujiridhisha ni nani aliyewauzia maeneo hayo wananchi hao.

Aidha Waziri Mpina amepiga marufuku ujenzi wa aina yoyote ile usifanyike katika eneo hilo mpaka hapo serikali itakapotoa ripoti ya uchunguzi huo ambapo utafanyika ndani ya mwezi mmoja kuanzia sasa.

Jumla ya kaya Elfu tano (5,000) za wavamizi hao zimetambuliwa na zinakadiliwa kuwa na watu elfu 22,8000.

Vilevile baadhi ya Wafanyabiashara na wafugaji waliokuwepo mnadani hapo, wamemweleza Mhe Waziri wa Mifugo na Uvuvi kuwa mnada huo unakabiliwa na changamoto nyingi ikiwepo uchakavu wa Miundombinu ya kutunzia Mbuzi,Ukosefu wa Maji,Ubovu wa barabara iendayo mnadani hapo na uhaba wa maeneo ya kuchungia mifugo kutokana na Eneo la mnada huo kwa kiasi kikubwa kuvamiwa na wananchi.

Katika hatua nyingine Katibu Mkuu Mifugo Dkt Maria Mashingo amesema kuwa wamefa nikiwa kuipata hati ya mnada huo baada ya kuitafuta kwa muda mrefu sana.

"Eneo la mnada wa upili wa Pugu lina ekari 1,900,kutokana na uvamizi wa eneo hilo, mnada huo kwa sasa unakadiliwa  kuwa na eneo lililobaki kwa ajili ya matumizi sahihi ya mnada ni asilimia 25 tu.Hati ya eneo la mnada huo ilitolewa mwaka 1939 na serikali ya wakati huo"Alisema

Awali Waziri Luhaga Mpina alifika mnadani hapo majira ya saa kumi alfajiri akiambatana na Katibu Mkuu Mifugo Dkt. Maria Mashingo na baadhi ya Maafisa kutoka Wizarani.Kazi ya kwanza aliyoanza nayo mara tu baada ya kufika mnadani hapo ni kukagua Vibali (Movement Permit) katika makundi ya ng'ombe yote yalikuwepo kwa wakati huo.

Waziri mpina akiwa katika mnada wa Mbuzi Pugu alifanikiwa kumkamata mfanyabiashara mmoja wa Mbuzi aliyejulika kwa  jina la Zacharia Mabula (43) aliyekwepa kulipia ushuru wa Mbuzi 112 kati ya Mbuzi 228 aliokuwa nao.Kwa kutumia sheria taratibu na kanuni zinazoendesha mnada huo,mfanyabiashara huyo amepigwa faini ya Tsh.800,000/=

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe, Luhaga Mpina kushoto akiwa na Katibu Mkuu Mifugo Dkt. Maria Mashingo wakiangalia malisho ya ng'ombe katika mnada wa Pugu

Mhe. Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina akiangalia mbuzi alipotembelea mnada wa Pugu ivi karibuni.

Mhe. Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina akiangalia ng'ombe akiwa mnadani

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni