Nav bar

Alhamisi, 19 Aprili 2018

WAZIRI MPINA APOKEA MADUME 11 YA NG'OMBE BORA KATIKA KITUO CHA NAIC - ARUSHA

Mhe.Waziri Luhaga Mpina akiwa na Katibu Mkuu Mifugo Dkt. Maria Mashingo akikata utepe kuashiria kupokelewa kwa Madume hayo ya Mbegu


Maelekezo ya Mhe. Waziri wakati alipokuwa akipokea madume ya ng'ombe bora 11 ya mbegu katika Kituo cha Uzalishaji Mifugo kwa Chupa (NAIC) Arusha.

1.Amemshukuru na kumpongeza KMM kwa kazi kubwa ya kuhakikisha utoshelevu wa mbegu za AI kwa kuwepo kwa jumla ya madume bora 26 hadi sasa yenye uwezo wa kuzalisha jumla ya dozi 3,120,000 kwa mwaka.

2.Amemuagiza KMM kuandaa mpango maalum wa kuhimilisha Ng'ombe Milioni moja wa maziwa.Mpango huo uanze kutekelezwa katika bajeti ya mwaka huu(2018/19). 

3.Pia Mhe. Waziri amemuagiza KMM kufanya tathmini ya kuona kama kuna haja  au umuhimu wa kuagiza maziwa na mazao yake nje ya nchi.Tathimini hiyo inatakiwa kukamilika katika kipindi cha wiki mbili kuanzia sasa. 

4.Aidha Mhe. Waziri amemuagiza KMM  kufanya tathmini ya kuona kama maziwa na mazao yake yanayoingizwa nchini yanaingia kwa kufuata taratibu zote za kisheria. Tathmini hiyo  pia ifanyike ndani ya wiki mbili kuanzia sasa.

5.Mhe. Waziri ameonya wafanyabiashara wote Wanaoingiza bidhaa za maziwa na mazao yake kwa njia za magendo, kuacha mara moja.Serikali itafanya ukaguzi na itachukua hatua kali za kisheria kwa mfanyabiashara yoyote atakayebainika.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni