MAABARA YA KISASA YA UTAFITI KATIKA SEKTA YA UVUVI NCHINI YAJENGWA KUPITIA MRADI WA SWIOFISH
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Sekta ya Uvuvi, Dkt. Rashid Tamatamah amesema serikali imetilia mkazo suala la utafiti katika sekta ya uvuvi nchini ili kuhakikisha inapata taarifa sahihi ya maeneo ya mavuvi, kuzalisha vifaranga bora vya samaki pamoja na chakula bora cha samaki. Akizungumza jijini Dar es Salaam wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa maabara ya kisasa ya utafiti wa uvuvi itakayotumika na Taasisi ya Utafiti Uvuvi Tanzania (TAFIRI) inayojengwa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kupitia Mradi wa Usimamizi Shirikishi wa Rasilimali za Uvuvi Kusini Magharibi mwa Bahari ya Hindi (SWIOFISH), Dkt. Tamatamah amesema mradi huo unaofadhiliwa na Benki ya Dunia kwa mkopo wa masharti nafuu wa Shilingi Bilioni 2.6 unalenga kukuza sekta ya uvuvi nchini. “Kwenye uchumi wa bluu katika awamu hii tunategemea kununua meli nane kwenye uvuvi wa bahari kuu hivyo unapofanya uvuvi wa bahari kuu haujiendei tu lazima watafiti kama TAFIRI waende baharini wajue chambo wana...