Nav bar

Jumanne, 30 Septemba 2025

MIFUGO NA UVUVI YAANZA KIBABE SHIMIWI 2025

◼️ Yawararua Maadili 2-0 Kamba Wanaume

◼️Yatwaa Magoli 40 na pointi 2 Mpira wa pete baada ya Maendeleo ya Jamii kutokomea kusikojulikana

Timu za mchezo wa Kamba upande wa Wanaume na Mpira wa pete kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi zimeanza vema kampeni ya kuwania ubingwa wa michuano ya SHIMIWI 2025 baada ya kuibuka na ushindi kwenye michezo yao ya leo Septemba 01,2025 iliyofanyika jijini Mwanza.

Nyota njema kwa Timu hizo ambazo zimekuwa gumzo jijini Mwanza tangu zilipoingia ilianza kwa upande wa mchezo wa kuvuta Kamba Wanaume ambapo walipimana ubavu na timu ya Tume ya Maadili na kufanikiwa kuibuka na ushindi wa mivuto yote miwili.

Baada ya ushindi huo kikosi cha wachezaji wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kilielekea kwenye uwanja wa CCM Kirumba kulikofanyika mchezo wa mpira wa Pete baina yao na timu ya Maendeleo ya jamii ambayo ilipotea ghafla na kumlazimu mwamuzi wa mchezo huo kuipa timu ya Mifugo na Uvuvi ushindi wa magoli 40-0 na pointi 2.

Kampeni ya kusaka ubingwa wa Michuano hiyo kwa Upande wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi itaendelea kesho ambapo timu ya soka itachuana na timu ya Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, kamba wanawake wakimenyana na timu ya Ofisi ya Makamu wa Rais, kamba wanaume wakichuana na UCSAF  na mpira wa pete kivumbi kitakuwa baina yao na timu ya Tume ya Utumishi.




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni