Nav bar

Jumanne, 20 Mei 2025

WATAALAMU KUTOKA NIGERIA KUJIFUNZA UCHUMI WA BULUU TANZANIA

Na. Hamisi Hussein - WMUV, Dodoma

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Bw. Abdul Mhinte, amesema kuwa Tanzania inaendelea kutekeleza sera ya kukuza Uchumi wa Buluu kwa kutumia rasilimali zake nyingi ambazo zimekuwa chachu ya maendeleo ya uchumi huo.

Bw. Mhinte ameyasema hayo leo, Mei 20, 2025, alipokuwa akiikaribisha kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara, Prof. Riziki Shemdoe,  timu ya wataalamu kutoka Taasisi ya Mafunzo ya Sera na Mipango Kitaifa ya Nigeria (NIPSS), ambayo imewasili nchini kwa ziara ya mafunzo juu ya masuala ya Uchumi wa Buluu.

“Nchi yetu ina rasilimali nyingi zinazochochea maendeleo ya Uchumi wa Buluu, zikiwemo bahari, maziwa na mito, ambazo zimekuwa zikitumika kukuza na kuendeleza sekta hii muhimu,” amesema Bw. Mhinte.

Ameeleza kuwa sekta ya uvuvi inatoa fursa nyingi, na kusisitiza utayari wa Wizara kushirikiana na wadau mbalimbali katika kuendeleza sekta hiyo kama sehemu ya mpango mpana wa kukuza Uchumi wa Buluu.

Kwa upande wake, Kiongozi wa msafara huo ambaye ni Naibu Mkuu wa Jeshi la Polisi mstaafu kutoka Nigeria, Bw. Leye Oyebade, ameishukuru Wizara kwa juhudi inazoendelea kuzifanya katika kukuza Uchumi wa Buluu kupitia sekta ya uvuvi.

Timu hiyo ya wataalamu kutoka NIPSS imeanza ziara yao nchini Tanzania kwa lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu katika masuala ya uchumi wa buluu.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi ( Mifugo) Bw. Abdul Mhinte (Kulia) akipokea Zawadi Kutoka Naibu Mkuu wa Jeshi la Polisi Mstaafu kutoka Nchini Nigeria (Kushoto) walipofika Ofisi za Wizara kwa ajili ya Ziara ya kujifunza juu ya masuala ya uchumi wa Buluu Mei 20, 2025 , Mtumba Jijini Dodoma

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi ( Mifugo) Bw. Abdul Mhinte (Kulia) akisisitiza Jambo wakati akiongea na Timu ya Watalaamu Kutoka Nigeria (haipo Pichani) iliyokuja Nchini kwa Ziara ya kujifunza masuala ya Uchumi wa Buluu, Mei 20, 2025 , Mtumba Jijini Dodoma

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi ( Mifugo) Bw. Abdul Mhinte (Katikati) Kwa Niaba ya Katibu Mkuu akizungumza na timu ya wataalamu kutoka nchini Nigeria walipofika Ofisi za Wizara kwa ajili ya Ziara ya kujifunza juu ya masuala ya uchumi wa Buluu Mei 20, 2025 , Mtumba Jijini Dodoma

Naibu Mkuu wa Jeshi la Polisi Mstaafu Nchini Nigeria Bw. Leye Oyebade akizungumza na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi ( Mifugo) Bw. Abdul Mhinte wakati wa timu ya wataalamu kutoka nchini humo walipofika Ofisi za Wizara kwa ajili ya Ziara ya kujifunza juu ya masuala ya uchumi wa Buluu Mei 20, 2025 , Mtumba Jijini Dodoma

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi ( Mifugo) Bw. Abdul Mhinte ( wa Tano, Kulia) akiwa kwenye Picha ya Pamoja na timu ya Wataalamu kutoka nchini Nigeria walipofika Ofisi za Wizara kwa ajili ya Ziara ya kujifunza juu ya masuala ya Uchumi wa Buluu Mei 20, 2025 , Mtumba Jijini Dodoma

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi ( Mifugo) Bw. Abdul Mhinte (Katikati) akiwa kwenye Picha ya Pamoja na timu ya wataalamu kutoka nchini Nigeria walipofika Ofisi za Wizara kwa ajili ya Ziara ya kujifunza juu ya masuala ya uchumi wa Buluu Mei 20, 2025 , Mtumba Jijini Dodoma


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni