Nav bar

Jumanne, 3 Agosti 2021

BODI YA NYAMA YATAKIWA KUANZISHA MFUMO WA KUWATAMBUA WANENEPESHAJI MIFUGO

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi mheshimiwa Abdallah Ulega ameiagiza Bodi ya Nyama nchini kuanzisha mfumo utakaosaidia wafugaji kunenepesha mifugo yao ili waweze kunufaika zaidi na fulsa za masoko ya ndani na nje ya nchi kwani mahitaji ya nyama ni makubwa.

 

Amesema hayo wakati akizungumza katika mkutano maalumu na wafugaji wa kienyeji, wafugaji wa kisasa pamoja na taasisi wezeshi za wafugaji wafuge kibiashara ili waweze kutoshereza soko la ndani na soko kubwa la nje ya nchi katika ukumbi wa Mvuvi house jijini Dar es salaam.

 

Mheshimiwa Ulega alisema elimu ya kutosha iendelee kutolewa ili kuwajengea uwezo wa kunenepesha mifugo yao hata wafugaji wa kienyeji katika ng’ombe, mbuzi na kondoo wao wa asili maana taifa limepata fulsa kubwa huko katika nchi za uarabuni hivyo mahitaji ya nyama ni makubwa.

 

Alisema katika halmashauri zote nchini wafugaji wa fundishwe namna moja ya kunenepesha na kuzalisha kwa wingi mifugo yao huku wakijua soko la ndani na nje ya nchi linachotaka ili kupata nyama yenye ubora na yenye thamani ya kimataifa itakayompa mfugaji faida kubwa.

 

Akizungumzia wafugaji kukopesheka kwenye mabenki ya mifugo nchini Mheshimiwa Ulega alisema Wafugaji waingie mikataba na wenye viwanda vya kuchakata nyama kwa namna wanavyowasambazia mifugo yao ili wapate thamani ya kuweza kukubalika na kuaminiwa kupata fulsa za fedha katika mabanki hayo.

 

“Mikataba watakayopata itakuwa sehemu ya wao kukubalika Wafugaji wapate fedha kwenye mabanki wanenepeshe mifugo yao wauze kimataifa wapate pesa maana biashara ni nzuri sana” alisema Mheshimiwa Ulega.

 

 Alisema lengo kubwa likiwa ni kuwajengea uwezo wafugaji  kuzalisha kiwango kikubwa cha nyama kitakachoweza kutoshereza mahitaji ya soko la ndani na soko la nje ya nchi katika ubora wa nyama iliyoandaliwa vyema.

 

“Ukiandaa vizuri nyama yako mteja akiiona ni nzuri na yenye ubora utafanya biashara maana soko lipo” alifafanua.

 

Hatahivyo Naibu Waziri huyo alisema hadi sasa viwanda vya kuchakata nyama za ng’ombe, mbuzi na kondoo nchini bado vinazalisha chini ya viwango vya idadi iliyohitajika kuzalisha katika viwanda hivyo kutokana na kukosekana kwa idadi kubwa ya mifugo hiyo hivyo aliwataka watanzania kutumia vyema fulsa hiyo kwa kufuga kwa wingi ilikuweza kutoshereza soko.

 

Aidha Mheshimiwa aliitaka pia bodi hiyo ya nyama kutafuta namna ya kufundisha wafugaji wa asili wabadilike kwa kufuga kisasa zaidi hata kuachana na ufugaji wa kuzurulisha mifugo bali uwe ni ufugaji katika ubora na viwango vya kimataifa katika mashamba yao ya ufugaji.

 

Naye Afisa manunuzi wa Tanchoice cha kibaha mkoani Pwani Jabil Mohamed alisema kiwanda chao kinauwezo wa kuchinja mbuzi 4500 kwa siku na ng’ombe 1000 kwa siku lakini mpaka sasa wanapata idadi ya mifugo chini ya idadi wanayohitaji kulingana na uwezo wa kiwanda ambapo wanachinja mbuzi hadi 2000 kwa siku na ng’ombe 150

 

“Jambo ambalo uzalishaji wetu bado ni kiwango kidogo sana sawa na asilimia 20 cha kiwanda chetu hivyo kiwanda hicho ni fulsa kwa wafugaji kwani inaweza kuwatoa kwenye umasikini hadi mafanikio ya utajiri” alisema Jabil.

 

Jabil alisema kiwanda hicho mpaka sasa kina vibali vya kupeleka nyama katika nchi tano duniani.


Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega akizungumza na wadau wa bodi ya nyama kwenye kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa Uvuvi house jijini Dar es Salaam ambapo amewataka wadau hao kutumi fursa ya biashara ya Mifugo iliyopo huku akiitaka Bodi ya Nyama Tanzania kuhakikisha inawatambua wadau wake. (02.08.2021)


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni