Nav bar

Jumamosi, 24 Julai 2021

WATENDAJI SEKTA ZA MIFUGO NA UVUVI WAWEKWA KITIMOTO

Na Mbaraka Kambona,


Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mashimba Ndaki amewataka Watendaji wanaofanya kazi ya ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali katika Minada, Mialo na Vituo vya Ukaguzi kufanya kazi hiyo kwa uaminifu na uadilifu huku akionya kuwa hawataweza kuendelea kuwa na Mtendaji atakayejihusisha na vitendo vinavyosababisha upotevu wa mapato ya Serikali.


Waziri Ndaki aliyasema hayo katika kikao cha Tathmini ya Ukusanyaji wa Maduhuli ya Serikali kwa mwaka uliopita na kuweka malengo mapya ya ukusanyaji mapato kwa mwaka 2021/ 2022 kilichofanyika jijini Dodoma Julai 23, 2021.


Akiongea na Watendaji hao aliwaeleza bayana kuwa ili waweze kufikia malengo ya kukusanya Shilingi Bilioni 90 walizojiwekea kukusanya kwa mwaka huu wa fedha ni lazima wafanye kazi hiyo kwa uaminifu na uadilifu kinyume na hapo hawatafanikiwa kufikia malengo.


"Katika kipindi ambacho nimekuwa hapa Wizarani nimepata taarifa nyingi kuhusu baadhi yenu kujihusisha na vitendo vya upotevu wa mapato, acheni kufanya hivyo kwa sababu tukikugundua hatutaweza kuendelea na wewe," alisema Ndaki


Aliongeza kuwa kumekuwa na vitendo vingi vya upotevu wa maduhuli ya Serikali ambavyo  vimekuwa vikifanywa na baadhi ya maafisa  wasiokuwa waaminifu na  kupelekea serikali kutopata mapato yanayostahili.


Waziri Ndaki aliendelea kusema kuwa Mhe. Rais, Samia Suluhu Hassan amewaahidi Watanzania mambo mengi mazuri na  ili mambo hayo yaweze kutekelezeka yanahitaji pesa, na miongoni mwa pesa zinazotegemewa na Serikali ni pamoja na zile zinazokusanywa kutoka kwenye minada, mialo na vituo vya ukaguzi.


Aliendelea kubainisha kuwa kwa mwaka huu atafuatilia kwa karibu utendaji kazi wa watendaji hao na amepanga kukutana nao kila robo mwaka ili kupima utendaji kazi wa kila mmoja ili kuona kama yale malengo yaliyowekwa yanafikiwa.


"Nitaendelea kuwatembelea katika vituo vyenu vya kazi, nitakuja kwa taarifa na wakati mwingine bila taarifa na nikifika nitataka kujua mmefikia wapi kuhusu ukusanyaji wa maduhuli," alisisitiza Ndaki


Aidha, Waziri Ndaki aliwaelekeza Watendaji hao kupelekea taarifa ya minada isiyo rasmi ili aitambue na kuifuta  kwa sababu imekuwa ni kikwazo kwa minada inayotambulika kisheria.


 Pia aliwasisitiza Watendaji hao kuendelea kufanya kazi ya Serikali kwa haki ikiwa ni pamoja na kuzuia uvuvi haramu na utoroshaji wa mifugo kwani vitendo hivyo vimekuwa ni sehemu ya upotevu wa mapato ya Serikali.




Kaimu Mkurugenzi, Uzalishaji na Masoko (Mifugo), Steven Michael akifafanua jambo katika kikao cha Tathmini ya Ukusanyaji wa Maduhuli kwa mwaka uliopita na kuweka malengo ya ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali kwa mwaka mpya wa fedha 2021/ 2022 kilichofanyika jijini Dodoma Julai 23, 2021.


Afisa Mfawidhi Msimamizi wa Rasilimali za Uvuvi Kanda Kuu ya Tanganyika, Juma Makongoro akitoa maoni yake katika kikao cha Tathmini ya Ukusanyaji wa Maduhuli kwa mwaka uliopita na kuweka malengo ya ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali kwa mwaka mpya wa fedha 2021/2022 kilichofanyika jijini Dodoma Julai 23, 2021.


Afisa Tehama, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Baltazari Kibola akitoa ufafanuzi kuhusu mifumo ya kielekroniki ya kukusanyia maduhuli ikiboreshwa vizuri inavyoweza kusaidia kutatua changamoto ya upotevu wa maduhuli ya Serikali katika kikao cha Tathmini ya Ukusanyaji wa Maduhuli kwa mwaka uliopita na kuweka malengo ya ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali kwa mwaka mpya wa fedha 2021/2022.


Mhasibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Richard Mayongela akiwasilisha taarifa ya makusanyo ya maduhuli ya mwaka uliopita na mipango ya ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali kwa mwaka mpya wa fedha 2021/2022 kwenye kikao cha Tathmini ya Ukusanyaji wa Maduhuli ya Serikali kwa mwaka fedha uliopita na kuweka mipango ya ukusanyaji wa maduhuli kwa mwaka mpya wa fedha 2021/2022 kilichofanyika jijini Dodoma Julai 23, 2021.


Mhasibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Veronica Kishala akiwasilisha taarifa ya makusanyo ya maduhuli kwa mwaka wa fedha uliopita na mipango ya ukusanyaji wa maduhuli Serikali kwa mwaka mpya wa fedha 2021/2022 katika kikao cha Tathmini ya Ukusanyaji wa Maduhuli ya Serikali na kuweka mipango ya ukusanyaji kwa mwaka mpya wa fedha 2021/ 2022 kilichofanyika jijini Dodoma Julai 23, 2021.


Pichani ni sehemu ya Watendaji wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi walioshiriki Kikao cha Tathmini ya Ukusanyaji wa Maduhuli kwa mwaka wa fedha uliopita na kuweka malengo ya ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali kwa mwaka mpya  wa fedha 2021/2022 kilichofanyika jijini Dodoma Julai 23, 2021.


Wahasibu Wakuu wa Sekta za Mifugo na Uvuvi wakifuatilia matukio yanayoendelea kufanyika katika Kikao cha Tathmini ya Ukusanyaji wa Maduhuli kwa mwaka wa fedha uliopita na kuweka malengo ya ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali kwa mwaka mpya wa fedha 2021/ 2022. Kulia ni Richard Mayongela (Uvuvi) na kushoto ni Veronica Kishala (Mifugo).


Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mashimba Ndaki (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na sehemu ya Watendaji wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi waliohudhuria Kikao cha Tathmini ya Ukusanyaji wa Maduhuli kwa Mwaka wa fedha uliopita na kuweka malengo ya ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali kwa mwaka mpya wa fedha 2021/2022 uliofanyika jijini Dodoma Julai 23, 2021. Kulia waliokaa ni Kaimu Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Emmanuel Bulayi na Kushoto ni Kaimu Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Amos Zephania.



Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mashimba Ndaki (katikati) akimueleza jambo Kaimu Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Amos Zephania (kushoto) muda mfupi baada ya kumaliza Kikao cha Tathmini ya Ukusanyaji wa Maduhuli kwa mwaka uliopita na kuweka malengo ya ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali kwa mwaka mpya wa fedha 2021/ 2022. Kulia ni Kaimu Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Emmanuel Bulayi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni