Nav bar

Alhamisi, 14 Januari 2021

WAKAGUZI WA NGOZI WATAKIWA KUSIMAMIA UZALISHAJI WA NGOZI BORA

Mkurugenzi Msaidizi wa Mazao ya Mifugo, Usalama wa Chakula na Lishe, Bw. Gabriel Bura amewataka wakaguzi wa zao la Ngozi wa Kanda ya Mashariki kusimamia ubora wa Ngozi zinazozalishwa.

 

Bura ameyasema hayo leo (12.01.2021) wakati akifungua mafunzo ya siku mbili ya wakaguzi wa Ngozi wa Kanda ya Mashariki (Dar es Salaam, Pwani na Morogoro) yanayofanyika katika ukumbi wa Mvuvi House jijini Dar es Salaam.

 

Wakaguzi hao wa Ngozi wametakiwa kusimamia uzalishaji wa zao hilo katika hatua zake zote ili kupata Ngozi zinazofaa kusindikwa katika viwanda.

 

Aidha, wakaguzi hao wametakiwa kutumia sheria namba 18 ya mwaka 2008 inayolenga kuboresha zao la ngozi ili wadau waweze kuzalisha ngozi bora inayokidhi mahitaji ya viwanda vyetu na hatimaye kuwa na tija ya uzalishaji wa zao hilo.

 

Bura amesema uzalishaji wa ngozi za ng’ombe na mbuzi kwa siku ni vipande 31,000 lakini ni asilimia 10 tu ya ngozi zinazopelekwa viwandani hufaa kwa ajili ya kusindikwa, na asilimia 90 hazifai kutokana na kukosa ubora unaofaa kwa ajili ya kusindikwa.

 

“Hivyo baada ya kupata mafunzo haya ni matarajio ya wizara kuwa mtakwenda kulisimamia nyema zao hili la Ngozi ili kuhakikisha Ngozi yote inayozalishwa inakuwa bora,” alisema Bura.

 

Hapa nchini vipo viwanda viwili tu vyenye uwezo wa kusindika ngozi hadi hatu ya mwisho ambavyo ni Moshi Leather Industry chenye uwezo wa kusindika futi za Mraba elfu 15,000 kwa siku na Himo Tannery and Planter Ltd chenye uwezo wa kusindika futi za mraba 10,000 kwa siku.

 

Uwezo wa usindikaji wa viwanda vyote viwili kwa siku ni sawa na vipande 1000 vya ngozi ya ng’ombe na 9000 vya ngozi ya mbuzi, hivyo bado kuna uhitaji wa viwanda vya kusindika Ngozi na vilivyopo kuongeza uwezo wake wa kusindika zao hilo.

Kaimu Mkurugenzi wa Mazao ya Mifugo, Usalama wa Chakula na Lishe, Bw. Gabriel Bura (kulia aliyesimama) akifungua mafunzo ya siku mbili ya Wakaguzi wa Ngozi kutoka Hamashauri na Manispaa za Kanda ya Mashariki (Dar es Salaam, Pwani na Morogoro) yenye lengo la kuwajengea uwez, yanayofanyika katika ukumbi Mvuvi Huose Jijini Dar es Salaam (12.01.2021)


Mshiriki wa Mafunzo ya wakaguzi wa ngozi, Bw. Severine Munishi kutoka Halmashauri ya Malinyi akichangia mada ya Sheria ya Ngozi katika mafunzo ya kikao cha wakaguzi wa Ngozi yanayofanyika katika ukumbi wa Mvuvi House Jijini Dar es salaam. (12.01.2021)

Picha ya pamoja ya Washiriki wa Mafunzo ya siku mbili ya Wakaguzi wa Ngozi na Wawezeshaji nje ya Jengo la Mvuvi House Jijini Dar es Salaam. (12.01.2021)

Mtaalam wa Ngozi Mstaafu, Bw. Emmanuel Muyinga akiwasilisha mada ya Sheria ya Ngozi namba 18 ya mwaka 2008 kwa Washiriki wa Mafunzo ya Ngozi ya siku Mbili toka Halmashauri na Manispaa za Kanda ya Mashariki (Dar es Salaam, Pwani na Morogoro) yaliyofanyika katika ukumbi wa Mvuvi House Jijini Dar es Salaam. (12.01.2021)

Afisa Mifugo Mkuu kutoka Idara ya Uzalishaji na Masoko (WMUV), Bw. Edson Kilyenyi akitoa maelezo mafupi ya kuwakaribisha washiriki wa Mafunzo ya wakaguzi wa Ngozi kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi afungue mafunzo hayo, yanayofanyika katika ukimbi wa wa Mvuvi House Jijini Dar es Salaam. (12.01.2021)



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni