Nav bar

Ijumaa, 10 Julai 2020

MAONYESHO YA 44 YA KIMATAIFA YA BIASHARA "SABASABA" 2020


Mkurugenzi wa Idara ya Uzalishaji na Masoko (WMUV), Dkt. Felix Nandonde akiangalia ngozi iliyochakatwa alipotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika Maonesho ya 44 ya biashara (sabasaba) yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mwl. Nyerere, barabara ya Kilwa Jijini Dar es Salaam leo Julai 9, 2020. Kushoto wanaotoa maelezo kuhusu ngozi hiyo ni Wakufunzi wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo (LITA).



Mkurugenzi wa Idara ya Uzalishaji na Masoko (WMUV), Dkt. Felix Nandonde (kulia) akifurahia jambo na Maafisa wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi (TAFIRI) alipotembele banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika Maonesho ya 44 ya Kimataifa ya biashara (sabasaba) yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mwl. Nyerere, barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kushoto ni Lovette Mwansasu, na wa pili ni Hiari Chona. (09.07.2020)



Mkurugenzi wa Idara ya Uzalishaji na Masoko (WMUV), Dkt. Felix Nandonde (kulia) akimsikiliza Afisa Uvuvi Mkuu wa Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) alipotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika Maonesho ya 44 ya biashara (sabasaba) yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mwl. Nyerere, barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam. (09.07.2020)



Mkurugenzi wa Idara ya Uzalishaji na Masoko (WMUV), Dkt. Felix Nandonde (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Utafiti, Mafunzo na Huduma za Ugani, Dkt. Angello Mwilawa (wa pili kushoto), Afisa Mifugo Mkuu, Bezia Rwongezibwa (wa kwanza kushoto, Mtaalam wa Mifugo, Idara ya Huduma za Mifugo, Stanslaus Mchonde (wa kwanza kulia), Kaimu Meneja wa Shamba la Malisho Vikuge, Ally Karia (wa pili kulia) na Afisa Mifugo, Idara ya Uzalishaji na Masoko, Happyness Lyimo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni