Wadau wa tasnia ndogo ya ndege wanaofugwa wameipongeza Serikali kwa
kutatua kero za kisera ambazo zilikuwa zikidumaza tasnia hiyo.
Hayo yamesemwa na Katibu wa chama Kikuu cha Wadau wa Tasnia ya
Kuku (PAT), Manase Mrindwa katika kikao cha Wadau wa tasnia ya kuku kilichofanyika
jijini Dodoma Juni 18,2020.
Akiongea kwenye kikao hicho Mrindwa alisema kuwa bajeti
ya Serikali ya mwaka 2020/2021 imetoa majibu kwa kero zao kwa
kuondoa kodi kwenye mayai ya kutotolesha vifaranga yanayotoka nje ya nchi, imepunguza
tozo kwenye vyakula vya mifugo vinavyosafirishwa nje ya nchi na kupunguza
tozo kwenye mayai yanayosafirishwa nje ya nchi.
“Unafuu huu wa tozo tunategemea utaiinua tasnia hii ya ndege
wanaofugwa hapa Tanzania, alisema Mrindwa.
Pamoja na pongezi hizo Mrindwa alieleza changamoto zilizowakumba
kufuatia mlipuko wa maradhi ya Korona ambazo zimechangia kupungua kwa
ulaji wa bidhaa za kuku kutokana na mdororo wa biashara uliopelekea kufungwa
kwa baadhi ya shughuli za biashara ikiwemo mahoteli, migahawa, vyuo, shule na
kusitishwa kwa shughuli zinazoleta mikusanyiko ya watu.
"Kudumaa kwa biashara zinazohitaji mazao ya kuku, kupungua
kufuga kuliathiri viwanda vinavyozalisha vyakula vya mifugo, uingizaji wa
bidhaa za kuku kutoka nje zilisitishwa, wafugaji waliokopa kwenye taasisi
mbalimbali za kifedha walipata shida katika marejesho." Aliongeza Mrindwa
Aidha, Mrindwa alisema kuwa kufuatia kupungua kwa
changamoto ya mlipuko wa maradhi ya Korona shughuli za kibiashara
zimeanza kurejea katika hali yake jambo ambalo litasaidia kuimarisha biashara
hiyo huku akitaja shughuli ambazo zimeshaanza kurejea kama vile usafiri wa
anga, utalii, uzalishaji katika viwanda, mashamba ya kuku wazazi ambayo
yameanza kupokea vifaranga vya kuku na kuanza kuingia nchini virutubisho vya
kutengenezea vyakula vya mifugo.
Aliongeza kuwa kwa sasa wafugaji wameanza kuongeza
na kuimarisha shughuli zao za ufugaji hivyo kupelekea kuwa na changamoto
ya ongezeko la mahitaji ya vifaranga wa nyama na wa mayai.
"Serikali iendelee kujadiliana na nchi jirani hususani
Kenya na Zambia ili shughuli za mipakani ziweze kufanyika kama awali na
usumbufu wa madereva na ucheleweshwaji wa mizigo uishe ili kurahisisha
upatikanaji wa bidhaa za mifugo ili biashara iweze kuimarika zaidi, alisisitiza
Mrindwa.
Katika hatua nyingine, Wadau hao wamekiri kujifunza namna ya
kuweka mkakati wa kuimairisha ulaji wa nyama ya kuku na mayai hapa
nchini, kuhamasisha uanzishwaji wa viwanda vya kutengeneza dawa za kuku na
uwekezaji katika maghala na kuiomba serikali kuendelea na mchakato wa kuzalisha
soya ya kutosha kwa mahitaji ya vyakula vya mifugo.
"Hivi sasa kwa wastani Mtanzania mmoja anakula mayai 75 kwa
mwaka wakati kiwango cha FAO ni kula mayai 200 kwa mwaka, pia Mtanzania anakula
kilo 15 za nyama kwa mwaka wakati FAO inapendekeza kula kilo 45 kwa
mwaka." Alifafanua Mrindwa.
Wadau wa tasnia ndogo ya ndege wanaofugwa wameipongeza Serikali kwa
kutatua kero za kisera ambazo zilikuwa zikidumaza tasnia hiyo.
Hayo yamesemwa na Katibu wa chama Kikuu cha Wadau wa Tasnia ya
Kuku (PAT), Manase Mrindwa katika kikao cha Wadau wa tasnia ya kuku kilichofanyika
jijini Dodoma Juni 18,2020.
Akiongea kwenye kikao hicho Mrindwa alisema kuwa bajeti
ya Serikali ya mwaka 2020/2021 imetoa majibu kwa kero zao kwa
kuondoa kodi kwenye mayai ya kutotolesha vifaranga yanayotoka nje ya nchi, imepunguza
tozo kwenye vyakula vya mifugo vinavyosafirishwa nje ya nchi na kupunguza
tozo kwenye mayai yanayosafirishwa nje ya nchi.
“Unafuu huu wa tozo tunategemea utaiinua tasnia hii ya ndege
wanaofugwa hapa Tanzania, alisema Mrindwa.
Pamoja na pongezi hizo Mrindwa alieleza changamoto zilizowakumba
kufuatia mlipuko wa maradhi ya Korona ambazo zimechangia kupungua kwa
ulaji wa bidhaa za kuku kutokana na mdororo wa biashara uliopelekea kufungwa
kwa baadhi ya shughuli za biashara ikiwemo mahoteli, migahawa, vyuo, shule na
kusitishwa kwa shughuli zinazoleta mikusanyiko ya watu.
"Kudumaa kwa biashara zinazohitaji mazao ya kuku, kupungua
kufuga kuliathiri viwanda vinavyozalisha vyakula vya mifugo, uingizaji wa
bidhaa za kuku kutoka nje zilisitishwa, wafugaji waliokopa kwenye taasisi
mbalimbali za kifedha walipata shida katika marejesho." Aliongeza Mrindwa
Aidha, Mrindwa alisema kuwa kufuatia kupungua kwa
changamoto ya mlipuko wa maradhi ya Korona shughuli za kibiashara
zimeanza kurejea katika hali yake jambo ambalo litasaidia kuimarisha biashara
hiyo huku akitaja shughuli ambazo zimeshaanza kurejea kama vile usafiri wa
anga, utalii, uzalishaji katika viwanda, mashamba ya kuku wazazi ambayo
yameanza kupokea vifaranga vya kuku na kuanza kuingia nchini virutubisho vya
kutengenezea vyakula vya mifugo.
Aliongeza kuwa kwa sasa wafugaji wameanza kuongeza
na kuimarisha shughuli zao za ufugaji hivyo kupelekea kuwa na changamoto
ya ongezeko la mahitaji ya vifaranga wa nyama na wa mayai.
"Serikali iendelee kujadiliana na nchi jirani hususani
Kenya na Zambia ili shughuli za mipakani ziweze kufanyika kama awali na
usumbufu wa madereva na ucheleweshwaji wa mizigo uishe ili kurahisisha
upatikanaji wa bidhaa za mifugo ili biashara iweze kuimarika zaidi, alisisitiza
Mrindwa.
Katika hatua nyingine, Wadau hao wamekiri kujifunza namna ya
kuweka mkakati wa kuimairisha ulaji wa nyama ya kuku na mayai hapa
nchini, kuhamasisha uanzishwaji wa viwanda vya kutengeneza dawa za kuku na
uwekezaji katika maghala na kuiomba serikali kuendelea na mchakato wa kuzalisha
soya ya kutosha kwa mahitaji ya vyakula vya mifugo.
"Hivi sasa kwa wastani Mtanzania mmoja anakula mayai 75 kwa
mwaka wakati kiwango cha FAO ni kula mayai 200 kwa mwaka, pia Mtanzania anakula
kilo 15 za nyama kwa mwaka wakati FAO inapendekeza kula kilo 45 kwa
mwaka." Alifafanua Mrindwa.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni