Nav bar

Jumatatu, 15 Oktoba 2018

KATIBU MKUU MIFUGO AFANYA UKAGUZI MINADA YA SHANWA MASWA NA MWANUZI MEATU




Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof.Elisante Ole Gabriel leo amefanya ukaguzi mnada ya Awali wa Shanwa uliopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Maswa na Mwanuzi katika Halmashauri ya Wilaya ya Meatu.

Akiongea na Katibu Mkuu, Dkt. Gabriel Bura kutoka Wizarani ambaye pia ni mmoja wa timu Nzagamba, Dkt. Bura,amemweleza Katibu Mkuu kuwa tangu wamewasili hapo, kazi zinaenda vizuri bila shida yoyote.

Katibu Mkuu tangu timu Nzagamba imeanza kutekeleza majumu yake,katika mnada wa Senai timu ilifanikiwa kukusanya jumla ya Tsh.7,028,000/= ukilinganisha na Tsh.756,000/= zilizokuwa zinakusanywa kabla ya Nzagamba kuanza kutekeleza Majukumu yake. alisema.

Aidha Bura amesema kuwa wafanyabiashara wameanza kuelewa mabadiliko ya tozo mpya,isipokuwa bado kuna changamoto chache, baadhi ya wafanyabiashara wanafanya biashara nje Minada kinyume cha sheria ili kukwepa kwa Makusudi kulipa tozo zilizowekwe kisheria.

Wakati huo huo baadhi ya wafugaji waliokuwepo katika mnada wa Shanwa Maswa walitoa baadhi ya changamoto wanazokabiliana nazo kuwa ni pamoja na kupigwa faini pale Ngombe wanapofika pungufu katika mnada wa Kizota au Pugu hata kama atakuwa amekufa njiani kwa kukanyagwa na wenzake.

Akijibu baadhi ya changamoto zilizotolewa na wafugaji na Wafanyabiashara hao, Katibu Mkuu Mifugo Prof. Ole Gabriel aliwambia wafugaji/Wafanyabiashara hao kuwa ni vyema kufuata taratibu na kanuni zilizowekwa kwa mujibu wa sheria ili waweze kufanya biashara zao za mifugo bila bugudha yoyote.

Katika hatua nyingine Dkt. Benezeth Lutege akiwa katika Mnada wa awali wa Mwanuzi Halmashauri ya Wilaya ya Meatu,amemwambia Katibu Mkuu kuwa zoezi la ukusanyaji ushuru kwa kutumia tozo mpya liliingia dosari baada ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu kugoma kukusanya ushuru huo kwa kutumia tozo mpya kwa kisingizio cha kutokupata Taarifa hizo Mapema.

Mkuu nililazimika kutumia nguvu kuwatangazia wafugaji na Wafanyabiashara kuwa wanatakiwa kulipa viwango vipya vya tozo vilivyopitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mwaka huu wa fedha na sio vya Mwaka jana. ;alisema.

Katibu Mkuu akimsikiliza kwa makini Bw. Adam Noti, Afisa Mifugo katika Halmashauri ya Wilaya ya MASWA (Aliyenyoosha mkono)

Katibu Mkuu akiwa na badhi ya Wafugaji na wafanyabiashara wa Mifugo katika Mnada wa Shanwa Halmashauri ya Wilaya ya MASWA.

Katibu Mkuu Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel akiwa katika Mnada wa Shanwa katika Halmashauri ya Wilaya ya MASWA

Katibu Mkuu akiongea na baadhi ya wafanyabiashara waliopanga foleni wakisubiri kulipia tozo mbalimbali.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni