Nav bar

Alhamisi, 23 Agosti 2018

WAFUGAJI WAKUMBUSHWA KUFUGA KISASA




Wafugaji Mkoani Mwanza wametakiwa kufuga kisasa ikiwa ni pamoja na kuwa na mifugo ya kutosha ili kuweza kupata tija na kufikia uchumi wa viwanda.
                                                                                         
Akiongea na wadau mbalimbali wa mifugo katika mnada wa Nyamatara Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza hivi karibuni, Katibu Mkuu Wizara ya  Mifugo na Uvuvi, Profesa Elisante Ole Gabriel amewataka wafugaji kujifunza mbinu bora za ufugaji ili sekta ya mifugo iweze kutoa mchango stahiki katika upatikanaji wa Mali ghafi za viwandani.

Aidha Profesa Elisante amewataka wafugaji na wadau wote wa sekta ya mifugo kufata sheria za nchi katika kutekeleza shughuli zao ili kuepusha migongano baina yao na mamlaka mbalimbali za nchi.

Hata hivyo profesa Elisante Ole Gabriel amewahakikishia wafugaji kwamba serikali kupitia Wizara ya mifugo itahakikisha matatizo mengi ya wafugaji yanatatuliwa kwa wakati ili waweze kufanya kazi zao vizuri.

Pia amesisitiza kuwepo kwa matumizi ya mizani ya kupimia ng’ombe na sio kuuza kwa kuangalia ukubwa wa ng’ombe kwa macho ambapo itasaidia mfugaji na mnunuzi, na kuwepo na ushirikiano wa karibu kati ya Wizara, wafugaji na wanunuzi wa mifugo ili kuweza kufanya kazi zao katika utaratibu unaoeleweka.


Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi,kitengo cha Mifugo Profesa Elisante Ole Gabriel akiwa katika mnada wa Nyamatara Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza.

Profesa Elisante Ole Gabriel akiongea na wafugaji katika mnada wa Nyamatara Mkoani Mwanza


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni