Nav bar

Jumatano, 24 Desemba 2025

"SITACHOKA KUWASEMEA, KUWAPAMBANIA VIJANA WA KITANZANIA" - MHE. NG'WASI

 Na, Hamisi Hussein, Singida 

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi  ambae pia ni Mbunge wa Kundi la Vijana kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe. Ng'wasi  Damas Kamani, amesema  ataendelea kulisemea, kulitetea na kulipambania kundi la vijana kupata fursa mbalimbali za kujiinua kiuchumi hususani katika sekta ya mifugo na uvuvi.

Mhe. Ng'wasi  ameyasema hayo leo Desemba, 24, 2025, Wilayani Iramba Mkoani Singida, alipomwakilisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba katika Kikao cha Baraza la Kawaida la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) wilayani humo.

  "Pamoja na majukumu haya niliyopewa sitachoka kumtetea, kumsemea na kumpambania kijana wa kitanzania, lakini pia hata katika sekta hii ninayoisimamia huku ndio nitaweka nguvu zaidi ili ikiwezekana na sekta zingine ziige  kutoka kwetu namna ya kumsaidia kijana wa kitanzania"amesema N'gwasi.

Katika hatua nyingine Mhe. Ng'wasi amesema yuko tayari kushirikiana na vijana katika kuzifikia fursa za kiuchumi na kuwahimiza vijana hususani wa Chama cha Mapinduzi kuwa mstari wa mbele katika kukemea vitendo vya uvunjifu wa amani nchini pamoja na kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

"Mhe. Rais Samia ametuamini vijana na ametupa nafasi ili masuala yanayohusu vijana tuyaamue wenyewe, ni jukumu letu kumuombea Rais wetu na taifa letu kwa ujumla,kukemea  hadharani vitendo vya uvunjifu wa amani vinavyofanywa na baadhi watu" aliongeza Mhe. Ng'wasi.

Awali akisoma taarifa ya Chama  Katibu wa  UVCCM Wilaya ya Iramba  Bw. Amani Daudi amesema zaidi ya vikundi  31 vimenufika na fedha za asilimia 10 za halmashauri ambapo jumuiya ya umoja wa vijana imepata shilingi miloni 207.7.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng’wasi Kamani (wapili, kushoto) akikabidhi hati ya pongezi kwa umoja wa vijana  wakati wa kikao cha baraza la umoja wa vijana Wilaya ya Iramba, Mkoani Singida Desemba 24, 2025.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng’wasi Kamani akizungumza na viongozi wa chama cha Mapinduzi wa Wilaya ya Iramba, mkoani Singida Desemba 24, 2025.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng’wasi Kamani akisaini Kitabu cha wageni katika Ofisi ya Chama cha Mapinduzi Wilaya Wilaya ya Iramba Mkoani Singida mara baada ya kuwasili  kwa ajili ya kikao cha baraza la umoja wa vijana Desemba 24, 2025.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng’wasi Kamani akizungumza kwa niaba ya Waziri Mkuu wa Tanzania na Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba wakati wa kikao cha baraza la umoja wa vijana wilayani humo Desemba 24, 2025.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng’wasi Kamani akizungumza na Vijana wa UVCCM Wilaya ya Iramba kwa niaba ya Waziri Mkuu wa Tanzania na Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba wakati wa kikao cha baraza la umoja wa vijana wilayani humo Desemba 24, 2025.

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Iramba Bi. Emiliana Samson akizungumza wakati wa kikao cha baraza la umoja wa vijana wilayani humo Desemba 24, 2025.

Baadhi ya Vijana wa UVCCM Wilaya ya Iramba wakimsikiliza Mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng’wasi Kamani akizungumza kwenye kikao cha baraza la umoja wa vijana wilayani humo Desemba 24, 2025.





Hakuna maoni:

Chapisha Maoni