Nav bar

Jumatano, 16 Julai 2025

DKT. MHEDE AFUNGUA MKUTANO WA WADAU WA TASNIA YA KUKU

Na. Hamis Hussein 

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Edwin Mhede amefungua Mkutano wa tasnia ya Kuku (National Poultry Delivery Lab) unaofanyika  katika Hoteli ya Serena, Jijini Dar-es-salaam kuanzia leo Julai 15-16, 2025. 

Mkutano huo umelenga kuwakutanisha wadau wa tasnia ya kuku ili kuchambua, kujadili na kutoa suluhisho ya namna ya kukabiliana na changamoto zinazopunguza ufanisi na ushindani wa tasnia ya Kuku nchini.

Akifungua Mkutano huo,  Dkt. Mhede alielezea kuwa tasnia ya kuku  imeajiri asilimia 65 ya vijana na asilimia 51 ya wanawake nchini

 "Tasnia ya Kuku inachagiza ukuaji wa sekta nyingine ikiwemo Kilimo kutokana na mahitaji makubwa  ya vyakula vya Kuku vinavyotokana na mahindi na soya  ambayo vimeifanya tasnia hii  ya kuku kuwa ya kimkakati nchini" alisema Dkt. Mhede.

Aidha, Dkt Mhede amewahimiza Washiriki wa mkutano huo kutumia jukwaa hilo kuchambua na kuanisha maeneo ya kimkakati ambayo yatatatua changamoto zinazoikabili tasnia hiyo pamoja na  kujenga uwezo kwa wafugaji  na wafanyabiashara  wa tasnia ya kuku ndani ya nchi ili waweze kuzalisha kwa tija na kuyafikia masoko.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Edwin Mhede akifungua Mkutano wa tasnia ya Kuku (National Poultry Delivery Lab) unaofanyika  katika Hoteli ya Serena, Jijini Dar-es-salaam kuanzia leo Julai 15-16, 2025.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Edwin Mhede, akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki mara baada ya uzinduzi  wa Mkutano wa National Poultry Delivery Lab  unaofanyika katika hoteli ya Serena, jijini Dar es Salaam kuanzia Julai 15-16, 2025.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Edwin Mhede akiwa katika mazungumzo na wadau kutoka Benki ya Dunia,  SAGCOT, pamoja na Shirika la IFAD kando ya Mkutano wa National Poultry Delivery Lab unaofanyika katika Hoteli ya Serena, jijini Dar es Salaam kuanzia Julai 15- 16, 2025.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni