Nav bar

Jumapili, 16 Mei 2021

KIKAO CHA MAKATIBU WAKUU WA NCHI ZA JUMUIYA YA MAENDELEO YA NCHI ZA KUSINI MWA AFRIKA (SADC) WENYE DHAMANA YA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI.


Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Rashid Tamatamah (katikati) akiongoza ujumbe wa Tanzania katika kikao cha makatibu wakuu wa nchi za Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) wenye dhamana ya  kilimo, mifugo na uvuvi. Kulia kwake ni Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bw. Andrew Massawe na Katibu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel wakiwa kwenye maandalizi ya mkutano wa mawaziri wa SADC utakaofanyika Tarehe 07 Mei 2021. Mkutano huo umefanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma. Mkutano huo unafanyika kwa njia ya video na kuhudhuriwa na nchi wanachama wa SADC. (05.05.2021)

Wajumbe kutoka Tanzania wakiwa katika kikao cha makatibu wakuu wa nchi za Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) wenye dhamana ya  kilimo, mifugo na uvuvi, kwa ajili ya maandalizi ya mkutano wa mawaziri wa SADC utakaofanyika Tarehe 07 Mei 2021. Ujumbe wa Tanzania umehudhuria mkutano huo kwenye ukumbi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma. Mkutano huo unafanyika kwa njia ya video na kuhudhuriwa na nchi wanachama wa SADC. (05.05.2021)

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Rashid Tamatamah (kushoto) ambaye anaongoza ujumbe wa Tanzania katika kikao cha makatibu wakuu wa nchi za Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) wenye dhamana ya  kilimo, mifugo na uvuvi, akibadilishana mawazo na Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bw. Andrew Massawe (katikati) na Katibu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel kwa ajili ya maandalizi ya mkutano wa mawaziri wa SADC utakaofanyika Tarehe 07 Mei 2021. Ujumbe wa Tanzania umehudhuria mkutano huo kwenye ukumbi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma. Mkutano huo unafanyika kwa njia ya video na kuhudhuriwa na nchi wanachama wa SADC. (05.05.2021)

Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Sera na Mipango kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Bw. Adam Mwaigoga (katikati), Afisa Uvuvi Mwandamizi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bw. Didas Mtambalike (kulia) na Mkurugezi wa Idara ya Sera na Mipango kutoka Wizara ya Kilimo Bw. Obadiah Nyagiru wakibadilishana mawazo kabla ya kuanza kwa kikao cha maandalizi ya mkutano wa mawaziri wa nchi za Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) wenye dhamana ya  kilimo, mifugo na uvuvi, utakaofanyika Tarehe 07 Mei 2021. Ujumbe wa Tanzania umehudhuria mkutano huo kwenye ukumbi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma. Mkutano huo unafanyika kwa njia ya video na kuhudhuriwa na nchi wanachama wa SADC. (05.05.2021)


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni