Nav bar

Jumatatu, 29 Februari 2016

MKUTANO WA UWASILISHAJI WA MAELEZO YA BOTI ZA KISASA ZA DORIA KUTOKA ITALY

Baadhi ya wajumbe  wa wajumbe wa mkutano wakisikiliza maelezo kutoka kwa Mh Wsaziri wa KMU( hayupo pichani)


 Waziri wa KMU  Mh. Mwigulu Nchemba akitoa maelezo kwenye mkutano














Mkuu wa jeshi la Polisi Tanzania (IGP) Ernest Mangu akiwa kwenye mkutano huu




Mkurugenzi wa uvuvi katika Wizara ya KMU bwana Hosea Gonza Mbilinyi wa tatu kutoka kulia akimsikilza kwa makini mkuu wa jeshi la polisi







Waziri wa KMU Mh Mwigulu Nchemba akitoa maelezo kuhusu umuhimu wa boti hizo kwa ajili ya doria 




Katibu Mkuu wa Wizara ya KMU (Uvuvi) Dr Yohana Budeba  kushoto akiwa na Mkurugenzi wa uvuvi Bw Hosea Gonza Mbilinyi kulia



Wataalam kutoka kampuni ya  CMESCOMMANDMULTROLE-ULCRAFASTPACROLOAT kutoka kushoto ni Bw Aleksandr Zinrman na Bw Francisco Gargiulo



Boti ya kisasa ya doria aina ya CMES 40 yenye uwezo wa kukimbia zaidi ya KM 160 kwa saa inayotarajiwa kununuliwa ikiwa kazini




Bw Francisco Gargiulo kutoka kampuni ya CMESCOMMANDMULTROLE-ULCRAFASTPACROLOAT kutoka Italy inayotengeneza boti hizi akitoa maelezo kuhusu boti hii

Jumanne, 23 Februari 2016

TRAINING WORKSHOP FOR THE STANDARD OPERATING PROCEDURES SOPs FOR EPIDEMIOLOGICAL, LABARATORY AND COMMUNICATION HELD AT GIRAFFE OCEAN VIEW HOTEL 22 - 23/02/2016

AU and  INTERAFRICAN Bureau for Animal Resource members take a picture  together with veterinary officers from different countries at giraffe hotel in Dar es salaam


Mr. James wabacha a Project Coordinator talks about the Standard Method and Procedure in Animal Health SMP - AH project

 
Dr. Joram Mghwira - Assistant  Director in Transboundary animal disease control at Ministry of  Agriculture,Livestock and Fisheries and  Focal Point of SMP - AH project addressing participants during opening of SOPs workshop 

Focal Point of this project Mr. Masambu explains about the role of SOPs in laboratory testing and diagnosis
Discussing on reviewing of the SOPs

Jumatatu, 22 Februari 2016

MKUTANO WA WAZIRI WA KILIMO,MIFUGO NA UVUVI MHE.MWIGULU NCHEMBA ULIOFANYIKA 21/02/2016 KATIKA KIJIJI CHA DIHOMBO WILAYANI MVOMERO




Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi  Mhe.Mwigulu Nchemba akisaini kitabu cha wageni baada ya kufika katika kijiji cha Dihombo wilani Mvomero




Mhe.Waziri  Mwigulu Nchemba akiteta jambo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo,Mifugo na Uvuvi Mhe Dr.Maria Mashingo katikati ni Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Bi.Betty Mkwassa.


       Baadhi ya wanachi wa vijiji vya Dihombo na                Kambala wakiwa tayari eneo la mkutano






Katibu Tawala wa Wilaya ya Mvomero Bi Veronika  Kinyemi akimkaribisha Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe.Betty Mkwassa

Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mh.Betty Mkwassa akiwakaribisha wageni waliofika katika mkutano huo
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo,Mifugo na Uvuvi Dr.Maria Mashingo akitambulisha wageni aliofuatana nao kutoka Wizarani

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Bw.George Lucas Mkindo akieleza mikakati waliyojipangia ili kutatua mgogoro wa wakulima na wafugaji




Mbunge wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Mhe.Sulman Ahmed Sadiq akiongea na wanachi wa Jimbo hilo




Mkuu  wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Dr.Rajabu Rutengwe akimkaribisha Mhe.Waziri ili azungumze na Wananchi.






Waziri wa Kilimo,Mifugo na Uvuvi Mhe.Mwigulu Nchemba akiwahutubia wanachi wa Vijiji vya Dihombo na Kambala



Wananchi wakimsikiliza waziri,hayupo Pichani





Mzee Iddi Ally wa kijiji cha Dihombo akimweleza Waziri juu ya uvamizi wa shamba lake lenye Ekari zaidi ya 20 lililovamiwa na Wagaji.







Mkurugenzi wa Uzalishaji Mifugo na Masoko Bi.Anuciata Njombe akiteta jambo na Katibu Mkuu Dr.Maria Mashingo katika kijiji cha Kambala.



Ijumaa, 19 Februari 2016

MAAFISA WA WIZARA YA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI WALIOPANDISHWA VYEO KUANZIA TAREHE 01/02/2016 KWA NGAZI MBALIMBALI KWA SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI.



Benard N.Kaali- Mkuu wa kitengo cha Habari na  Mawasiliano Serikalini(HGCU)


Dkt.Joram E.Mghwira -Mkurugenzi msaidizi wa Udhibiti wa Magonjwa ya Mlipuko ya Wanyama na Ukaguzi wa mifugo na mazao ya mifugo.

Herman Lyimo-Mkuu wa kitengo cha Sheria(HLU)



Nezarlon Israel kitosi-Mkurugenzi  msaidizi huduma za Ugani na Usajili wa Mifugo

UJUE MPANGO BUNIFU WA MODENIZASHENI WA SEKTA YA MIFUGO ULIOTAMBULISHWA KWA WADAU WA SEKTA YA MIFUGO KATIKA KANDA 7 ZA TANZANIA BARA


Mpango wa Modenaizesheni ya Sekta ya Mifugo imelenga kuleta mageuzi makubwa yatakayoifanya sekta hii kuwa na mchango chanya hivyo kuchangia zaidi katika pato la taifa, kuyakabili mahitaji ya soko na tija kiuchumi, kijamii na uhifadhi wa mazingira kwa maendeleo endelevu. Mkakati huu umelenga kuzivuna fursa katika sekta za nyama, maziwa na kuku kwa kuimarisha usimamizi wa mnyororo mzima wa thamani ili kukabiliana na umaskini pamoja na kufanya maboresho katika usalama wa chakula, upatikanaji malisho bora, ubora wa vinasaba kwenye mifugo asilia, kupunguza migogoro baina ya makundi ya wakulima, waf ugaji na hifadhi, uhakika wa maji na virutubisho vinginevyo. 

Mkakati unalenga pia kutoa majibu ya changamoto za vinasaba katika mifugo asilia, ufugaji na uthibiti wa magonjwa, uwepo wa masoko ya uhakika, ubora na usalama katika bidhaa za mifugo na uongezaji thamani katika bidhaa za mifugo. Mkakati utakaoratibu mahitaji yote ya kisera, kisheria, kiuchumi na kimkakati hivyo kupelekea ustawi na ubora wa sekta ya mifugo mageuzi kutoka ufugaji wa mazoea kuwa wa kisasa, wenye kuleta tija, kuhifadhi mazingira, kuinua viwango vya lishe kwa maendeleo endelevu ya jamii na taifa kwa ujumla kwa kufanya yafuatayo:- 

(i) Kuwawezesha wafugaji kwa kuwapa teknolojia za kisasa, 
ujuzi na elimu bora ya ufugaji 
(ii) Kuwezesha upatikanaji wa huduma za ugani na pembejeo 
(iii) Kuimarisha miundombinu ya masoko ya mifugo na bidhaa za mifugo 
(iv) Kuwawezesha wafugaji, jamii za wafugaji na sekta binafsi kuwa na mchango zaidi 
(v) Kuimarisha taasisi za kitaifa na serikali za mitaa kuweka ukisasa katika sekta ya mifugo 
(vi) Kuboresha mifumo ya kitaasisi na kisera katika uwekezaji ili kuweka mazingira bora ya kuvutia uwekezaji baina ya seri- 
kali na sekta binafsi. 

Muundo wa Mpango wa Modenization.  

Mpango wa modenaizesheni ya Sekta ya Mifugo unalenga kutekeleza Sera ya Taifa ya Mifugo ya mwaka 2006 katika muktadha wa Dira ya Taifa ya miaka mitano, Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP), Kilimo Kwanza, Mkakati wa Taifa wa Kukuza Uchumi 
na kuondoa Umaskini (MKUKUTA), 

Vipaumbele: 
1. Kipaumbele cha kwanza ni :- 

(i) Mkakati wa Kuanzisha maeneo maalumu ya malisho katika Vijiji: Mkakati huu unalenga kuanzisha na kuhifadhi maeneo ya malisho katika vijiji kama ilivyo kwa maeneo ya hifadhi ya misitu ya vijiji. 

(ii) Uimarishaji vinasaba assilia (Sus- tained Genetic gains in Tanzania Livestock breed) 

(iii) Kuimarisha ufugaji wa ng’ombe wa nyama 

(iv) Kuimarisha ufugaji wa  kuku 

(v) Kuimarisha ufugaji wa ng’ombe wa maziwa 

(vi) Kuimarisha masoko ya ndani na nje ya nchi 

(vii) Kuimarisha mifumo ya vet erinari ili kuhakikisha afya na 
usalama kwa mifugo na binadamu .

(viii) Kuboresha tafiti na huduma za ugani kwa kuimarisha mifumo ya mawasiliano ya kisasa .

(ix) Kujenga jamii za wafugaji zilizo imara .

(x) Kupunguza migogoro ya ardhi na kuhifadhi mazingira (Conflict to coexistence: Livestock & Con- servation) 

(xi) Kichocheo katika uwekezaji kwa maendeleo ya sekta ya mifugo .

(xii) Kuhuisha Mpango wa maendeleo wa sekta ya mifugo katika mpango wa taifa wa maendeleo ya sekta ya kilimo na maendeleo vijijini .

(xiii) Masuala mtambuka Uhifadhi na usimamizi wa malisho  Kuna msukumo mkubwa wa wa magugu na mimea mingine inayoendelea kuharibu mifumo ya ikolojia hivyo kuathiri malisho asilia. Ongezeko la shughuli za kibinadamu na wingi wa mifugo unaombatana na uharibifu mkubwa wa mazingira na pia harakati za uhifadhi wa ardhi vimepelekea migogoro ya mara kwa mara katika maeneo mengi nchini. 

Takribani asilimia 2% ya ardhi inayofaa kwa malisho (hekta milioni 1.28) inamilikiwa na serikali za vijiji katika mpango wa matumizi bora ya ardhi ambao umetekelezwa na vijiji chini ya asilimia 10% katika wilaya 81 kati ya wilaya 150. Vile vile,aina 
23 kati ya aina 30 za magugu vamizi zilizogundulika nchini Tanzania yameathiri zaidi maeneo ya malisho hivyo mifumo imara ya ikilojia ni nguzo muhimu kwa uzalishaji wa mifugo asilia na ile ya kisasa. Kwa kutambua kuwa zaidi ya asilimia 50% ya kaya za Tanzania zinafuga, suala la malisho linasta- hili kupewa kipaumbele kikubwa hivyo jukumu la kwanza na la msingi katika mkakati huu wa modenaizesheni ni kutafuta na kuimarisha malisho bora.

Mkakati huu utazingatia sheria na kanuni zilizopo na zitakazotungwa pia zikisimamiwa ipasavyo. 


Jumatano, 17 Februari 2016

WADAU WA SEKTA YA MIFUGO WATAMBULISHWA MPANGO BUNIFU WA KUENDELEZA SEKTA YA MIFUGO TANZANIA KANDA YA NYANDA ZA JUU KUSINI (MIKOA YA IRINGA, MBEYA,RUKWA NA RUVUMA M

Wadau wa Sekta ya Mifugo wa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini (Mikoa ya Iringa, Mbeya, Ruvuma na Rukwa) nWakitambulishwa Mpango Bunifu wa Sekta ya Mifugo ,Mkutano uliofanyika Ukumbi wa Benjamin Mkapa Mbeya






Wadau wa Sekta ya Mifugo wa Mkoa wa Mbeya Wakiwa Katika Picha ya Pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Dkt Maria Mashingo Mwenye Miwani Katikati

Wadau wa Sekta ya Mifugo wa Mkoa wa Iringa Wakiwa Katika Picha ya Pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Dkt Maria Mashingo  Mwenye Miwani Katikati


Wadau wa Sekta ya Mifugo wa Mkoa wa Ruvuma  Wakiwa Kwenye Picha ya Pamoja na Katibu Mkuu Dkt Maria Mashingo na Mshauri Elekezi wa Mpango Bunifu Dkt Kaush Arha Nje ya Ukumbi wa Benjamin Mkapa Mbeya